Haya Ndiyo Madhara Ya Utoaji Wa Huduma Ya Hovyo

Kila mmoja wetu ni mtoa huduma yaani kila mtu kuna kitu anauza kwa mwingine kwa lugha rahisi.Kwa sababu sisi ni binadamu na tunaishi kwa kutegemeana. Kama ulikuwa hujui asilimia 85 ya mafanikio yako yanatoka kwa wengine na asilimia 15 tu inatoka kwako.Kwa maana hiyo basi, hata useme wewe ni jeshi la mtu mmoja ni ngumu …

Jitafakari, Je Kile Unachofanya Kitaweza Kukufisha Hapa?

Ni vema ukajitafakari mapema kama kile unachofanya kitaweza kukufikisha kule unakotaka kufika. Kila mmoja ana ndoto zake na kufanikiwa inategemea na kile unachofanya. Viko vitu vingine unavyofanya vinachangia kujirudisha nyuma. Kuna vitu kweli ukivifanya kwa hakika vitakurudisha nyuma na kuna vitu ambavyo ukivifanya vitakupeleka mbele. Ni muda wa kujipima kama kile unachofanya kweli kinakulipa? Na …

Huyu Ndiye Mwalimu Wa Vitu Vyote

Kila mtu anakuwa mgeni kwenye baadhi ya maeneo katika maisha yetu.Huwezi kuwa mwenyeji kwenye kila kitu. Kuna maeneo utakua vizuri na kuna maeneo hautakua vizuri lazima utawategemea wengine. Kila mtu anamtegemea mwingine ili maisha yake yaweze kwenda. Hakuna ambaye hamtegemei mwingine kwa sababu sisi ni viumbe vya kutegemeana. Kila ambaye alifikia kwenye ubobezi hapo mwanzo …

Njia Moja Ya Kuwa Na Maisha Mazuri Kati Njia 52

Mwandishi wa kitabu njia 52 za kuwa na maisha bora mwandishi Rolf Dobeli ametushirikisha katika kitabu chake. Kwenye kitabu cha Tano za Juma alichoandika mwandishi Makirita Amani ameweza kukichambua vizuri na hapa mimi leo ninakushirikisha njia moja ya kuwa na maisha mazuri. Njia hiyo ni, ” Unachoona kwa wengine na kukitamani, siyo bora kama unavyofikiria. …

Fedha Hazina Kitu Hiki Kimoja

Fedha ni jawabu la mambo yote kadiri ya kitabu cha mhubiri. Hakuna anayeweza kubisha kwamba fedha siyo ya muhimu ni muhimu kwani inatusaidia kupata kile tunachotaka. Fedha ni zao la thamani, kadiri unavyotoa thamani zaidi na wewe kipato kinaongezeka. Yaani ukitoa thamani zaidi na fedha inaongezeka. Ni kama vile unavyotoka jasho maana yake nishati inatoka …

Kama Unataka Kuuza Sana, Tumia Sheria Hii Ya Halber Kwenye Masoko

Kwenye kitabu cha barua kutoka gerezani mwandishi alikuwa anamwandikia mtoto wake wakati yeye akiwa gerezani.Alikuwa ana mshirikisha misingi mbalimbali ya mafanikio. Mwandishi anamshirikisha mtoto wake sheria ambayo alikuwa anaitumia kwenye masoko na kufanikiwa. Sheria hii tunaweza kuitumia hata sisi na ikatusaidia kupata masoko na kuongeza mauzo. Unajua mauzo ndiyo kila kitu katika biashara, kama huuzi …

Usiwalazimishe Wengine Kuwa Kama Wewe

Kifupi hatuwezi kufanana na pale tunapokazana wengine wawe kama sisi tunakua tunafanya kazi ambayo iko nje ya uwezo wetu. Usiwalazimishe wengine wawe kama wewe lakini pia usijione wewe ni bora kuliko wao. Lengo kubwa la kujifunza ni kuyafanya maisha yako kuwa bora na siyo kuwalazimisha wengine maisha yao kuwa bora. Utakapojifunza na maisha yako yatakapokuwa …

Vyovyote Utakavyojichukulia Uko Sahihi

Aliyewahi kugundua magari ya kifahari yanayojulikana kwa jina la Land cruiser V8 anayejulikana kwa jina la Henry Ford,Aliwahi kunukuliwa akisema,”Kama unafikiri unaweza au unafikiri huwezi uko sahihi.” Wewe unajifikiriaje? Unaweza au huwezi? Ukijichukulia unaweza uko sahihi na ukijichukulia huwezi uko sahihi pia. Yaani vyovyote vile unavyojichukulia uko sahihi. Wewe ndiyo mkurugenzi wa maisha yako, hivyo …

Hakuna Unachofanya Ambacho Kitakosa Matokeo Haya

Kuna vitu vingine viko nje ya uwezo wetu. Unaweza ukajituma kweli, ukachukua hatua ya ziada lakini kuna kitu ambacho huwezi kukipanga kitokeeje ambacho ni matokeo. Hakuna mwenye udhibiti wa matokeo, asili huwa inaamua matokeo na hakuna mtu wa kuipangia. Unapofanya kitu chochote kile, kuwa tayari kwa matokeo yoyote yale maana hatuna udhibiti wa matokeo gani …

Kabla Hujakutana Na Mtu Jifunze Mambo Haya Muhimu

Ukitaka kuwa mtu wa ushawishi sehemu yoyote ile pendelea kuwa mtu wa kujifunza watu wanataka nini. Wape kile wanachotaka na wewe utapewa kile unachotaka. Huwezi kuwashawishi watu kama wewe ni mtu wa kujali mambo yako na kusahau mambo ya wengine. Kama ni msomaji wa kitabu jitahidi usome kitabu cha how to win friends and influence …

Design a site like this with WordPress.com
Get started