Jiunganishe Na Kitu Hiki Kwa Gharama Yoyote Ile

Wakati mwingine huwa tunazingua ndiyo maana hatupati kile tunachotaka. Hupati kile unachotaka kwa sababu hujajiunganisha na kile unachotaka. Ujumbe muhimu sana ninaokusihi uondoke nayo hapa ni kwamba, nenda kajiunganishe na madhabu au altare ya kule unakotaka kufika. Kwa mfano, kama wewe unamwimini Mungu basi nenda kajiunganishe na altare au madhabu yake kwa gharama yoyote ile. …

Jifunze Kufanya Kitu Hiki Na Hutakua Na Maisha Magumu

Maisha yetu yametawaliwa na kuuza. Na wale wanaoweza kuuza vizuri ndiyo wanaofanikiwa sana. Huwezi kupokea kama huna unachotoa. Kila mmoja wetu kuna kitu anakiuza ndani yake iwe una biashara au umeajiriwa. Ukiwa umejiriwa unakuwa unauza vitu viwili muda na ujuzi wako. Kila mtu ana thamani inayomfanya aweze kulipwa vizuri. Shida ni kwamba thamani uliyonayo haiwezi …

Siku Zote Mambo Huwa Hayawi Hivi

Mambo hayawi kama vile unavyohofia. Unachokihofia wala huwa hakitokei. Usitengeneze hofu ambayo haipo katika uhalisia. Huna haja ya kuhofia kesho itakuwaje kwa sababu siyo jukumu lako. Kesho itakuja kama vile ilivyopangwa kutokea. Usihofie yajayo yatakuwaje, wewe fanya kile unachopaswa kufanya sasa, yajayo yatajipanga yenyewe. Wako ambao wanajipanikisha kwa kufikiria mambo yajayo yatakuwaje.Fanya yako na iachie …

Hizi Ndizo Nyakati Mbili Za Kupima Rafiki Wa Kweli

Tumeshazoea kusikia kwa watu kuwa rafiki wa kweli utamjua wakati ukiwa na shida. Hilo ni kweli na wala halina ubishi. Hata waswahili wanasema, akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli. Huwa tunapatwa na changamoto mbalimbali katika maisha yetu hivyo si ajabu yule ambaye unadai ndiyo rafiki wa kweli akaja kukuangusha. Wale waliosimama na wewe wakati …

Jinsi Ya Kufilisika Kimawazo

Kama unamaliza siku bila kuingiza maarifa mapya ni dalili ya kufilisika kimawazo. Kwa zama tunazoishi watu wengi wamevurugwa na maisha. Mitandao ya kijamii inawachosha watu kwa kufuatilia habari mbalimbali ambazo hata haziwasaidii kwenye maisha yao. Jitahidi angalau kila mwezi usome kitabu kinachoendana na eneo moja la maisha yako.Kile unachotaka kikue hakiwezi kukua kama wewe mwenyewe …

Rasilimali Mbili Muhimu Za Kuziheshimu

Kiufupi, hakuna mtu anayeweza kujitosheleza kwa kila kitu. Kila binadamu ana mtegemea mwingine ili maisha yaweze kwenda. Ni asili ya binadamu kutegemeana. Kujitegemea siyo kitu kibaya. Ni kizuri sana lakini huwezi kujitegemea kwa kila kitu, kuna eneo lazima utakua unahitaji msaada na huwezi kujitegemea kwa kila kitu. Kumbe basi, hakuna aliyeweza kusimama bila kutegemea wengine. …

Hiki Ndiyo Kitu Kinachowaumiza Watu Wengi

Hivi kati ya ujinga na ukweli kipi kinawaumiza watu wengi? Watu wengi huwa wanaumia kwa kuambiwa ukweli. Leo hii nakwenda kubadilisha mtazamo uliokuwa nao kwamba ukweli huwa haumuizi bali unamsaidia mtu. Aliyekuwa mtawala wa Roma, Marcus Aurelius aliwahi kunukuliwa akisema, ” kama kuna mtu anaweza kunishawishi na kunionesha kwamba nimekosea, nitafurahi na kuwa tayari kubadilika.Ukweli …

Kuwa Makini Na Kile Kilichokupandisha Juu

Rafiki yangu,Ulishawahi kujiuliza nini kitakachokuja kukushusha chini? Kilichokupandisha juu ndicho kitakachokuangusha chini. Hivyo kuwa makini sana na kile kilichokupandisha juu maana ndicho kitakachokuja kukuangusha chini. Angalia kwenye ndoa yako nini kilichofanya ndoa yako iwe juu? Basi kitakachokuja kukuangusha chini ni kile kilichokupandisha juu. Kilichokupandisha juu kwenye biashara yako ndicho kitakachokuja kukuangusha chini. Kuwa makini sana …

Hiki Ndiyo Kitu Pekee Kilichokufanya Ukubali Kushindwa Kwenye Kile Unachofanya

Kwanza nianze kukuambia kitu kimoja rafiki yangu, maumivu yamekuwa ni kikwazo kwa watu wengi kuweza kufikia mafanikio kwenye maisha yao. Wakati mwingine unajiuliza kwanini watu wengine wanafanikiwa licha ya kupitia maumivu makali? Nini kinachowafanya wavumilie maumivu wanayokutana nayo pale wanapotafuta kile wanachotaka? Chukulia mfano, wewe mwenyewe umewahi kufanya vitu vingapi ukashindwa au ukakata tamaa? Ni …

Jicheleweshe Kidogo Eneo Hili

Unatoka nyumbani vizuri huku ukiwa huna hata mpango wa kununua kitu. Lakini mara unakutana na mtu anayeuza viatu na viatu ni vizuri kweli yule muuzaji anakushawishi ununue na ulikuwa huna mpango huo. Unajikuta unaiingiwa na tamaa na kujiambia viatu ni vizuri nisipovichukua sitokuja kuvipata tena. Sasa pale unapojikuta umekipenda kitu na huna mpango wa kukinunua …

Design a site like this with WordPress.com
Get started