Jinsi Ya Kujiongezea Matatizo

Mpendwa rafiki yangu, Laiti kama kila mmoja wetu angekuwa anafanyia kazi yale anayoongea basi leo hii kila mmoja angekuwa na mafanikio makubwa. Tumekuwa ni watu wa kupanga na kuishia kuongea kwenye midomo yetu lakini hatuifanyii kazi yale malengo yetu. Tumekuwa ni watu kupika matatizo yetu sisi wenyewe. Tunajua nini tunatakiwa kufanya lakini hatufanyi. Kuepuka kufanya …

Jinsi Ya Kuwasha Moto Wa Hamasa Ndani Yako

Watu wengi wanaamua kufanya kitu fulani kwa sababu ya hamasa. Hamasa iliyoko ndani yetu ndiyo inatusukuma kuthubutu jambo fulani. Mara nyingi pale tunapokuwa na hamasa ya kazi fulani tunakuwa kama vile tuna moto ndani yetu unaowaka na hatuwezi kuuzima kwa kuongea bali kwenda kufanya kile ambacho kipo ndani yetu. Na muda mzuri wa kufanikiwa jambo …

Hili Ndiyo Eneo Ambalo Unapaswa Kujisalimisha ili Uweze kufanikiwa

Rafiki, Je umejitoa kweli kupata kile unachotaka? Je mafanikio makubwa unayotaka yanaendana na hatua unazochukua? Huenda unapenda mafanikio lakini matendo yako hayaendani na mafanikio. Unakuwa bado hujajisalimisha kwenye kile unachotaka. Ili uweze kufanikiwa unatakiwa kujisalimisha yaani, kujitoa kwenye kile unachotaka. Kama unataka kufanikiwa jisalimishe kwenye mambo ambayo yanahusiana na mafanikio. Jisalimishe kwenye kile unachotaka, kama …

Jifunze Kitu Hiki Kama Unataka Kufanikiwa

Rafiki, Wengi tunapenda kufanikiwa huku tukitaka tuendelee kubaki na maisha yetu ya mazoea. Mtu anataka kufanikiwa huku akitaka aendelee kulala sana, anataka kupunguza uzito huku akiendelea kula vile anavyotaka na hataki kufanya mazoezi. Kutaka mafanikio bila kulipia gharama ni ujinga wa hali ya juu sana. Hakuna matokeo unayoweza kupata bila kulipia gharama yake. Ukitaka kufanikiwa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started