Watu wengi husema, “Ubinadamu ni kazi.” Lakini ukweli ni kwamba, siyo kazi ngumu kama ukiamua kuishi kwa falsafa sahihi. Kwenye sura yake ya mwisho, Robin anatukumbusha kwamba dunia ya leo imejaa mashindano, presha, na maumivu yanayotufanya tusahau maana halisi ya ubinadamu — upendo, huruma, msamaha, na kujali. Ndiyo maana anatuongoza kurudi kwenye ubinadamu kwa falsafa …
ACHA KUAHIRISHA NDOTO ZAKO
Kila mtu ana picha fulani kichwani ya namna anavyotamani maisha yake yawe — ndoto ya biashara kubwa, nyumba nzuri, familia yenye furaha, au huduma inayogusa maisha ya watu wengi. Hizo ndoto ndizo zinatupa sababu ya kuamka kila asubuhi. Lakini bahati mbaya, wengi wamegeuka kuwa wapangaji wazuri wa kesho na wavivu wa leo. Kila siku tunasema: …
TUMIA VIZURI NAFASI YA PILI
Kuna nyakati tunapewa fursa nzuri sana za kufanya jambo ambalo linaweza kubadilisha maisha yetu kabisa. Tunahisi ndani ya mioyo yetu kwamba “hii ndiyo nafasi yangu,” lakini mara nyingi fikra zetu hutuzuia. Hofu huanza kuzungumza – “ukishindwa je?” “watu watakuonaje?” “labda siyo muda sahihi.” Mwisho wa siku, tunakaa kimya, tunachelewa kuchukua hatua, na ile fursa inapotea …
USIWE MJASIRI WA KUPOTEZA – KUWA MJASIRI WA KUJILINDA
Kuna kauli inayorudiwa sana na watu wengi: “Kama unataka kufanikiwa, lazima uchukue risk.”Ni kweli, lakini si kila risk ni ya busara.Wengi wameangamia si kwa sababu hawakuwa na ndoto, bali kwa sababu walikosa hekima ya kutofautisha kati ya risk nzuri na risk ya kijinga. Waliowahi kufanikiwa sana duniani — wajasiriamali wakubwa, wawekezaji, au viongozi — hawakuwa …
Continue reading "USIWE MJASIRI WA KUPOTEZA – KUWA MJASIRI WA KUJILINDA"
Kama Unataka Usife, Epuka Kwenda Hii Sehemu
Kuna maneno maarufu sana ya Charlie Munger, mbia wa Warren Buffett, aliyewahi kusema: “All I want to know is where I’m going to die, so I’ll never go there.”(Nachotaka kujua ni wapi nitaenda kufa, ili nisije nikaenda huko.) Hii ni kauli rahisi lakini yenye hekima kubwa kuliko vitabu vingi vya mafanikio.Munger anatuambia kwamba siri ya …
Continue reading "Kama Unataka Usife, Epuka Kwenda Hii Sehemu"
USIRUHUSU SIKU MBAYA IKUDANGANYE KWAMBA UNA MAISHA MABAYA
Joel Osteen aliwahi kusema, “Don’t let a bad day make you feel like you have a bad life.” — Usiruhusu siku mbaya ikudanganye kwamba una maisha mabaya. Ni kweli kabisa, kwa sababu mara nyingi tuna tabia ya kuharibu picha kubwa ya maisha yetu kwa sababu ya siku moja isiyokwenda vizuri.Tunapopitia siku mbaya — mambo yakagoma, …
Continue reading "USIRUHUSU SIKU MBAYA IKUDANGANYE KWAMBA UNA MAISHA MABAYA"
KUNA BARAKA KATIKA KILA DHORUBA – USIPOTEZE IMANI YAKO
Joel Osteen aliwahi kusema, “There is a blessing in every storm. Don’t lose your faith.” — Kuna baraka katika kila dhoruba. Usipoteze imani yako.Ni sentensi fupi, lakini ndani yake kuna hekima ya maisha ambayo kila mtu anayepitia nyakati ngumu anatakiwa kuishikilia kwa nguvu. Tanzania, kama sehemu nyingine duniani, inapitia nyakati za majaribu, hususan baada ya …
Continue reading "KUNA BARAKA KATIKA KILA DHORUBA – USIPOTEZE IMANI YAKO"
VITU VIDOGO VYA WEMA HUISHI MILELE
Kuna watu wengi leo wameacha kufanya mambo mazuri kwa sababu wanaamini hakuna anayejali. Wanafikiri wema wao unapotea, kwamba hakuna anayeshukuru, na kwamba hakuna maana ya kuendelea. Lakini huo siyo ukweli. Kila jambo jema unalofanya—hata kama ni dogo kiasi gani—huacha alama. Huishi kwenye mioyo ya watu. Robin Sharma anatushirikisha hadithi mbili zenye nguvu kuhusu hili. Ya …
ISHI MAISHA YAKO HALISI, SI YA KUSAKA SIFA
Kuna watu wengi sana duniani wanafanya mambo si kwa sababu wanaamini ndani yao ni sahihi, bali kwa sababu wanataka kukumbukwa. Wanajenga majengo, wanatoa misaada, wanatoa hotuba—lakini ndani yao, msukumo ni sifa na kumbukumbu watakayoacha baada ya kufa. Wanafanya mambo kwa ajili ya jina, si kwa ajili ya maana. Lakini ukweli ni huu: mambo ya kulazimishwa …
Continue reading "ISHI MAISHA YAKO HALISI, SI YA KUSAKA SIFA"
Kukutana na Muhammad Ali: Somo la Unyenyekevu wa Kweli
Kuna matukio madogo ambayo hubadilisha kabisa mtazamo wetu kuhusu maisha — na moja wapo ni hadithi hii ya Robin Sharma alipokutana na mpiganaji maarufu duniani, Muhammad Ali. Robin anasimulia kuwa alipokuwa mtoto, familia yao ilikwenda mapumzikoni. Wakiwa njiani, ghafla waliona gari lililokuwa likiendeshwa na Muhammad Ali, shujaa wa ndondi aliyetikisa dunia. Mama yake Robin aliguswa …
Continue reading "Kukutana na Muhammad Ali: Somo la Unyenyekevu wa Kweli"