Rafiki, Kwenye kila eneo la maisha yako, hakikisha unawashangaza watu.Je, unashangazaje watu sasa? Unawashangaza watu kwa kwenda hatua ya ziada. Unafanya kazi, kiasi kwamba wale unaofanya nao wanakuogopa. Yaani hakuna ambaye anaweza kuvaa viatu vyako. Yaani thamani yako ni kubwa kiasi kwamba hakuna anayekukupuuza wala kushindana na wewe. Washangaze watu kwa kuwahi kazini kila siku. …
Watu Wanapenda Uhakika
Sisi binadamu ni watu wasiwasi, tokea watu waliotutangulia tokea kale, walikuwa wanaishi katika mazingira ambayo yaliwafanya waishi kwa wasiwasi muda wote. Kulikuwa na wanyama wakali, hivyo watu walikuwa wanaogopa sana, wana wasiwasi na kifo hivyo wanapoona sehemu kuna dalili ya kifo lazima wafe na wasiwasi. Kila mmoja wetu ana wasiwasi juu ya jambo fulani, hata …
Ondoka Kwenye Ukomo
Rafiki, Hongera sana rafiki yangu nikupendaye kwa kufika hapo ulipo. Ni hatua fulani kuwa hapo ulipo, kwani siyo wengi ambao wamefika hapo ulipo. Sina uhakika kama itakufaa lakini, unaweza kwenda zaidi ya hapo. Hapo ulipo siyo kwamba ndiyo mwisho, ondoa nukta au mwisho ULIONAO na kuweka koma yaani maisha yanaendelea. Kuna wakati tunajiwekea nukta sisi …
Ukishaamua Kwenda Sehemu Hii Nenda
Rafiki, Ukishaamua kwenda juu, nenda juu na usirudi nyuma tena. Ukiamua kufanya jambo, fanya na usiwe na hali ya kujiuliza niende au nisiende, nifanye au nisifanye. Ukishaamua kwenda mbele nenda, usirudi nyuma tena. Kwenye maisha ukishakuwa na chagua la pili utaridhika katika kuwajibika na chaguo la kwanza. Kuwa na nia mbili, siyo nzuri. Mara zote …
Utaripoti Nini Leo?
Rafiki yangu nikupendaye, Maisha yetu ni ripoti. Ili uweze kuripoti ni lazima kwanza ufanye.Huwezi kuripoti kama huna ulichofanya. Na ili ripoti iwe nzuri ni lazima uwe na orodha ya mambo ya kufanya ndani siku yako. Chukulia kwamba kila siku unapoamka unatakiwa kwenda kufanya kile unachopaswa kufanya na jioni kutoa ripoti. Kama unajua kuna ripoti unapaswa …
Haya Ndiyo Madhara Ya Uongo Kusemwa Mara Nyingi
Rafiki yangu nikupendaye, Mwandishi mmoja aliwahi kusema, uongo ukisemwa mara nyingi, na kurudiwa rudiwa kila mara watu wanaanza kuuamini kama ukweli. Mpaka sasa umeshasikia uongo gani ambao umeshakuwa kweli kwako?Kwa mfano, uongo ambao umesemwa katika fedha ni kwamba, huwezi kuishi na kufanikiwa pasipo kukopa.Uwongo huu unasemwa mara nyingi kwenye jamii kiasi cha watu wengi kuamini …
Continue reading "Haya Ndiyo Madhara Ya Uongo Kusemwa Mara Nyingi"
Kemikali Inayofanya Wewe Ujisikie Vizuri Kwenye Tabia Fulani
Rafiki yangu nikupendaye, Jana tulijifunza kitu kinachofanya tabia kuwa sugu ni ile hali ya KURUDIA. Ukitaka tabia fulani iwe sehemu ya maisha yako basi rudia kuifanya kila wakati. Kitu Kikubwa Kinachofanya Tabia Kuwa Sugu KwakoUnafikiri kwa nini watu huwa wanapenda kurudia sana kile walichofanya na kuwa tabia? Ni kwa sababu ya kemikali ya Dopamine ndiyo …
Continue reading "Kemikali Inayofanya Wewe Ujisikie Vizuri Kwenye Tabia Fulani"
Kitu Kikubwa Kinachofanya Tabia Kuwa Sugu Kwako
Rafiki yangu nikupendaye,Huwa tunatengeneza tabia kisha tabia zinatutengeneza na kuwa sehemu ya maisha yetu. Na kile ambacho tunafanya sasa, kiwe ni kizuri au kibaya ni kwa sababu ya tabia tulizojijengea au tulizokuwa nazo. Hakuna kitu ambacho mtu anafanya halafu siyo tabia yake. Tuna tabia ambazo tunazo ni nzuri na kuna tabia ambazo tunazo siyo nzuri. …
Continue reading "Kitu Kikubwa Kinachofanya Tabia Kuwa Sugu Kwako"
Fuatilia Ahadi Zako
Rafiki, Kuna ahadi nyingi sana ambazo unazo mpaka sasa lakini ulizokamilisha ni chache sana.Ziko ahadi ambazo ukizifuatilia basi zitakusaidia sana wewe kupata kile unachotaka. Ziko ahadi ambazo ni za kuwafuatilia watu wengine. Na ziko ahadi ambazo ni za kujifuatilia wewe mwenyewe. Mambo yako huenda hayaendi vile unavyotaka kwa sababu ya ahadi ambazo umepewa lakini huzifuatilii.Ushindi …
Kuwa Na Hii Roho
Rafiki yangu nikupendaye, Kuna roho fulani nataka uwe nayo ndani yako, hiyo ni roho ambayo ukiwa nayo basi itakusukuma kupata makubwa zaidi. Watu wengi ambao wamepata mafanikio makubwa kwenye maisha yao, wana roho hiyo, hata wewe ukiwa nayo, lazima utajisukuma sana kwenye kila eneo. Na roho hiyo ni kutaka kufanya zaidi, unatakiwa kuwa na hali …