Jinsi sheria Ya Parkinson Inavyofanya Kazi Kwenye Maisha Yako

Mwanamafanikio, Sheria ya Parkinson inasema, huwa tunatumia kitu kadiri kinavyopatikana. Kwa mfano, mtu ukiwa na elfu 10 kwa ajili ya kula, utakula chakula elfu kumi. Na ukiwa na elfu tano kwa ajili ya kula utakula chakula cha bei hiyo. Sisi binadamu huwa tuna tabia ya kutumia kitu kadiri kinavyopatikana. Kama kinapatikana kwa wingi basi tutatumia …

Mengine Yanapaswa Kusubiri

Rafiki, Kama bado hujaweza kupata kile unachotaka kwenye maisha yako, peleka nguvu zako zote kwenye mambo yenye tija kwako.Na namba moja ikiwa ni lengo lako kuu unalolipambania. Unapambania lengo? Jibu ulilopata ndiyo linapaswa kuwa kipaombele chako cha kwanza..Kama kuna kitu kinakuja kwenye maisha yako na hakina mchango kwenye ndoto yako kubwa uliyonayo, kinaweza kusubiri kwanza.Mengine …

Ni Bora Kuonewa Wivu Kuliko Kuonewa Huruma

Fanya kazi kiasi na upate mafanikio makubwa. Hata watu wakuonee wivu ni sawa kuliko kutokufanya kazi na kuwa na maisha ya shida huku ukisubiria watu wengine wakuonee huruma. Usijionee huruma wala kuwasubiri watu wengine wakuonee huruma.Usipoteze muda kujionea huruma. Watu wengi wamekuwa wanapoteza muda wao kujionea huruma kwa ambayo yametokea kwenye maisha yako. Kamwe usijione …

Aina Tatu Za Kushindwa

Sisi binadamu tuna vitu vingi sana vinavyotuzuia tusiende mbele.Tunapenda kwenda mbele lakini tunakuwa tunajizuia sisi wenyewe kwa kukanyaga breki.Huwa tunafikiri tunaanza kushindwa tu kimatendo lakini siyo kweli. Tunashindwa kwa vitu vingi sana. Kiakili. Kabla hatujashindwa kwa vitendo, tunakuwa tayari tumeshindwa kiakili. Ukishaiaminisha kwamba akili yako huwezi, na kweli hutoweza. Kama unataka ushindi, jiandae kwanza kiakili, …

Jenga Sifa Hii Hapa Itakayokusaidia Kupata Kile Unachotaka

Ni watu wengi ambao walishapita kwako au walipendekezwa na watu fulani kuhusu wewe au mtu mwingine ili wapate huduma au kitu fulani. Siyo mara yako ya kwanza kusikia mapendekezo haya;Hana shida huyo, msaidie. Mpaka watu wakupendekeze kwa watu wengine ili upate huduma au kitu fulani hata kama huna malipo taslimu ujue kuna sifa au mtu …

Ili Kupata Unachotaka Lazima Ufanye Hiki

Rafiki, Wajibu wako mkubwa kwenye maisha yako ni kupata kile unachotaka hasa. Mafanikio ambayo tunayatafuta tutayapata kwa wengine.Kuna vitu ambavyo wewe unavitaka lakini mwingine anavyo.Hivyo basi, kupitia watu, ndipo malengo yetu yanaweza kutimia. Na ili kupata unachotaka, lazima uwasukume wengi wapandishe viwango vyao ili kufikia viwango vyako wewe.Kwa mfano hapa, kama una wateja ambao wanafanya …

Huhitaji Kila Mteja

Kwenye biashara huhitaji kila mteja anunue kwako. Watu wanafikiri kwamba kila mtu anaweza kuwa mteja wako. Lakini, kwenye biashara siyo kila mtu anaweza kuwa mteja wako.Kwenye biashara huhitaji kila mteja bali unahitaji mteja ambaye anajua thamani yako.Mteja anayeijua thamani yako, hawezi kujiuliza mara mbili kwako anunue au asinunue. Mteja anayeijua thamani yako huwa ananunua. Mauzo …

Fanya Kitu Hiki Kila Mahali Unapoenda

Rafiki, Fanya angalau kitu kimoja kuwa bora kila mahali unapoenda. Yaani unapoenda sehemu, uwaachie baraka au habari njema itakayowafanya watu hao waneemeke kupitia wewe. Usiende sehemu yoyote ile, ukaondoka hujabadili kitu chochote kikawa bora. Itakua haina maana yoyote ya wewe kuwepo eneo hilo. Kama umekutana na mtu hakikisha unamwacha akiwa bora kuliko alivyokuwa. Kazi yetu …

Ushindani Ni Mkali

Kama ushindani ni mkali jifunze kujitofautisha na wengine.Ukiwa chini huwezi kujua uhasilia ukoje. Ni mpaka pale utakapokua ndiyo utajua uhalisia ukoje. Hata mamlaka ya mapato ukiwa chini kwenye biashara, hawahangaiki na wewe.Ila pale utakapokua, ndiyo wataanza kukufuatilia. Ukiwa chini, watu wanakuwa hawana mpango na wewe.Unapokua sasa, ushindani unakuwa ni mkubwa sana kwako. Ukianza kukua, watu …

Jinsi Ya Kuwa Mbele Ya Wengine

Hakuna zama ambazo ni rahisi kufanikiwa kama zama hizi tunazoishi.Zama tunazoishi zina kila aina ya fursa za kukuwezesha wewe kufanikiwa. Ukitaka kuwa mbele ya wengine, basi kuwa mtu wa kujifunza.Ukishakuwa mtu wa kujifunza lazima utakua unajua vitu vingi kuliko wengine. Anguko linaanza pale unapokuwa mjuaji na kujiona wewe unajua zaidi na kuacha kujifunza zaidi. Hakikisha …

Design a site like this with WordPress.com
Get started