Ukijua Kitu Hiki Basi Umeshafanikiwa

Huwezi kutatua tatizo usilolijua, ukijua kile kinachokuzuia wewe kuwa hivyo ulivyo ni rahisi sana kupata suluhisho lake. Mtu mmoja alishawahi kusema, jua ni wapi ukienda utakufa na kisha epuka kwenda sehemu hiyo.Kwa lugha rahisi ni kwamba jua ni kitu gani ukifanya kitakuletea shida na kisha epuka kufanya kitu hicho. Jua nini ukifanya kinapelekea biashara yako …

Ni Bora Kuonewa Wivu Kuliko Kuonewa Huruma

Rafiki, Kila unapoamka asubuhi na umepata bahati ya kupumua, shukuru na kisha nenda kaitumie hiyo pumzi uliyopata vizuri sana. Usipojituma kwenye kitu chochote kile, utajiweka katika mazingira ya watu kukuonea huruma, kulingana na hali unayopitia unatengeneza mazingira watu wakusaidie kwa kutia huruma. Usikubaliane na hilo, pambana kuhakikisha unakuwa bora ili usije kupata fedhea ya kutaka …

Unapaswa Kuwa Na Hasira Hii

Mtakatifu Agustino wa Hippo, aliwahi kunukuliwa akisema, Mungu aliyekuumba pasipo wewe kupenda hawezi kukubadilisha pasipo wewe kupenda. Kwa kauli hiyo, tunajifunza kwamba, hapa duniani kuwa hivyo ulivyo sasa ni machaguo yako. Ukitaka maisha mazuri au mabaya ni maamuzi yako wewe mwenyewe.Hakuna mabadiliko yoyote yatakayokuja kwako pasipo wewe mwenyewe kupenda mabadiliko hayo. Ukiamua kuwa yoyote yule …

Kinachotoa Mrejesho Kuhusu Thamani Tunayotoa

Rafiki, Asili haina huruma kabisa na mtu, ikiamua kufanya inafanya vile inavyotaka. Kuna wakati unaweza ukaandaa na kutoa thamani juu ya kitu fulani lakini soko likakataa. Unakuwa na shauku kubwa katika mchakato wa kufikia malengo fulani lakini unapofika sokoni, soko linaamua tofauti na ulivyopanga. Tunapaswa kuelewa kwamba, tunaweza kujiandaa vizuri lakini soko likaamua vingine. Tunaweza …

Usiwe Na Makasiriko

Rafiki, Ukitaka maisha yako yaende vizuri, usiwe na makasiriko na maisha au mafanikio ya watu wengine. Hakuna kitu kinawazuia watu kufanikiwa kama kuchukia mafanikio ya wengine. Badala ya kuwachukia watu waliofanikiwa pambana na wewe uweze kufanikiwa kwa sababu inawezekana pia. Hivi unajua kwa nini masikini wengi huwa hawawi matajiri, kwa sababu wanawachukia matajiri, kwa sababu …

Usiogope Mabadiliko Kama Utakutana Nayo

Rafiki, Mabadiliko ni kitu ambacho hakikwepeki kwenye maisha, kama wewe utagoma kubadilika, basi mazingira yanayokuzunguka yatabadilika.Na pale unaposhtuka na kugundua mazingira yamebadilika, basi jua umeshaachwa nyuma. Watu wengi wamekuwa wanaogopa kufanya mabadiliko kwenye maisha yao kwa sababu mabadiliko ni magumu. Mabadiliko huwa yanaleta hali fulani ambayo hatujaizoea. Pia mabadiliko yanamaanisha kuachana na kitu ambacho mtu …

Huyu Ndiyo Mtu Unayepaswa Kujilinganisha Naye

Rafiki, Tumeshazoea katika maisha, kujilinganisha na wengine. Kujilinganisha na wengine siyo kipimo sahihi. Huwa tunakosea sana kwenye hili. Tunapaswa kujilinganisha na sisi wenyewe kadiri ya mchakato na hatua tunazochukua ndani yetu. Kinachotokea pale tunapojilinganisha na wengine ni kujichukia sisi wenyewe na kujiona hatuna tunachofanya.Na mara tu baada ya kujilinganisha, tunanyang'anywa furaha yetu yote na kubaki na …

Amini Lakini Thibitisha

Hakuna mtu ambaye ana alama usoni ya kuthibitisha kwamba yeye ni mwaminifu. Tunapaswa kuwaamini watu lakini tusiache kuthibitisha na kujiridhisha kwa yale ambayo tunapima kutoka kwao. Wako watu wengi tu wanalizwa kwa kuwaamini watu kirahisi, mtu akikuambia kitu, una amini tu bila shaka. Na hii inasababishwa na ile hali ya kwamba, kama sisi ni waminufu, …

Tegemea Kilicho Bora

Rafiki, Maisha tuliyonayo ni matokeo ya mategemeo ambayo tumekuwa nayo siku za nyuma.Hatupati tofauti na tunachotegemea. Pale unapoamini jambo linawezekana na kulifanyia kazi ipasavyo, dunia yote itakusaidia kufanya ndoto zako, malengo yako na mipango yako kuwa kwenye uhalisia. Kupata ushindi kwenye maisha yako unapaswa kuiandaa akili yako kupata ushindi. Kama unataka kupata matokeo mazuri, andaa …

Jinsi Ya Kuongeza ushawishi Kwa Wengine

Rafiki,Tunaweza kupata tunachotaka kwenye maisha yetu kama tutaweza kuwashawishi wengine kutupa kile tunachotaka kutoka kwao.Lugha ya ushawishi ni nzuri kwa sababu, kwenye maisha hatupati tunachostahili bali tunachoshawishi. Binadamu ni watu wa sifa kiasili, kama unataka kumshawishi mtu halafu ukaanza na kumkosoa lazima atashindwa kukubaliana na wewe. Katika maisha unaweza kukutana na watu ambao wanafanya vitu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started