Vitu Viwili Pekee Ambavyo Havifundishwi

Mpendwa rafiki, Kuna mambo ambayo tumeshazoea kufundishwa na muda mwingine kuna kuwa na maeneo mbalimbali ya kutolea elimu kama vile shule au vyuo mbalimbali. sasa licha ya kuwa na sehemu hizo za kufundishia basi kuna vitu viwili ambavyo huwezi kumfundisha mtu. Ndiyo, vitu hivyo huwezi ukaenda kukaa darasani na kusema sasa nimekuja kujifunza na kwanza …

Jaribu Kufanya Kitu Hiki Leo Na Anza Maisha Haya Ambayo Hujawahi Kuishi

Mpendwa rafiki, Heri ya mwezi aprili na pasaka pia. Leo wakristu wote duniani wanasherekea sikukuu ya kufa na kufufuka kwa Bwana wao Yesu Kristu hivyo natumia nafasi hii kuwatakia heri ya sikukuu ya pasaka kwa wote na msherekee kwa amani na utulivu. Mpendwa rafiki , huenda tulikuwa tumekufa kimwili, kiroho na hata kiakili kwanini sasa …

Jinsi Wanandoa Wananvyowekana Uchi Hadharani Na Kuleta Matokeo Hasi Katika Mahusiano Ya Ndoa

Mpendwa rafiki, Hata siku moja mti hauwezi kuangushwa kwa shoka moja. Ukiona mpaka mti unaanguka chini basi ujue umekatwa na shoka zaidi ya mara mbili. Hata katika maisha yetu ya kawaida ukiona mpaka mtu anafikia mahali anakata tamaa juu ya kitu fulani basi ujue kuna sababu nyingi zilizomfanya aamue kukata tamaa. Kwa asili duniani hakuna …

Anayesema Hana Kitu Hiki Ni Muongo

Mpendwa rafiki, Wiki hii nilikuwa najitafakarisha mwenyewe baada ya kusoma makala ya mwandishi mwenzangu Makirita Amani aliyoandika kwamba watu wanakosea sana kujiambia kauli mbaya katika fedha na matokeo yake huwa inawanyima au kuwawekea ukuta wa kutopata fedha zaidi. Kauli ya kusema natafuta fedha imekuwa ikiwanyimwa watu wengi sana kupata fedha. Utawasikia watu wengi tu bwana …

Huu Ndiyo Uwezo Mkubwa Wa Kila Kiongozi Anaopaswa Kuwa Nao

Linapokuja suala la uongozi  watu wanaanza kufikiria  viongozi wengine badala ya kuanza kujifikiria kwanza yeye kama kiongozi. Kila mtu ni kiongozi hata kama huna unaao waongoza lakini si unajiongoza mwenyewe. Uongozi umetawala kila sehemu ya maisha yetu kuanzia ngazi ya familia mpaka ngazi ya taifa. Kama uko hai huwezi kukwepa kuongoza au kuongozwa kwa sababu …

Haya Ndiyo Makosa Makubwa Tunayofanya Kwenye Maisha Yetu

Kuna ule wimbo ambao kila mmoja wetu anapenda kumwimbia mwenzake au yeye mwenyewe pale tu anapoona mambo yamekwenda ndivyo sivyo. Wimbo wenyewe siyo mwingine bali ni shukuru kwa kila jambo. Lakini watu wengi wamekuwa wanautumia ndivyo sivyo huu msemo kwa kushukuru tu mambo mazuri lakini mabaya hapana. Rafiki, binadamu tumekuwa ni watu waliokosa shukrani na …

Kauli Mbaya Ya Kujiambia Kwa Mwanamafanikio Yeyote Yule

Mpendwa msomaji,Mtu aliyekataa tamaa na maisha ni mtu hatari sana. Hana tofauti na mtu anayetembea na dumu la petrol kwani muda wote anaweza akakulipua. Watu ambao unapaswa kukaa nao mbali kabisa ni watu ambao wamekatamaa ya maisha na wale ambao hawajipendi. Kuna wengine mpaka wanaamua kukufuru uumbaji wa Mungu wanasema ni bora wangezaliwa  mbwa ulaya. …

Usikimbizane Na Kitu Hiki Utakuwa Mtumwa

Kuna kipindi huwa ni kipindi cha kujenga maisha yaani kama ni nyumba basi unakuwa unajenga msingi. Vivyo hivyo hata katika maisha yetu kuna muda ni wa kutafuta na kuna muda wa kuvuna au kutumia. Karne hii ya ishirini na moja kumekuwa na uteja, uraibu wa aina nyingi, ukiacha wa mitandao ya kijamii basi kitu kingine …

Hawa Ndiyo Watu Wanaofurahia Maisha Hapa Duniani

Maisha ni furaha na wala siyo kuvumilia. Tumezaliwa kufurahia maisha na siyo kuvumilia maisha. Unaishi mara moja tu hapa duniani kama unashindwa kufurahia sasa usitegemee kama utakua na kipindi cha pili kama vile mpira wa miguu. Rafiki,Kuwa na furaha ni uamuzi wa mtu kuchagua na wala siyo kwenda kununua dukani. Ni kitu ambacho kipo ndani …

Njia Adimu Ya Kuongeza Mahusiano Imara Na Mwenzi Wako Wa Ndoa

Mpendwa rafiki, Huwa nasisitiza sana kusoma vitabu kwani kusoma vitabu kuna faida kubwa kwenye kila eneo la maisha yetu. Hata nikisema nikuandike faida za kusoma Vitabu itakuwa ni litania ndefu yaani orodha ndefu. kitu pekee ambacho ningeweza kukushauri kama hujui faida za kusoma vitabu basi anza kusoma vitabu utaona faida utakazozipata. Kama uko kwenye magrupu …

Design a site like this with WordPress.com
Get started