Jinsi Ya Kumkataa Shetani Na Mambo Yake Yote

Miongoni mwa viumbe waliopendelewa hapa duniani ni bindamu. Binadamu tumepewa nguvu ya kutawala kila kitu katika maisha yetu, sisi ndiyo tuna uwezo hata wa kutawala viumbe vingine. Kuna kitu cha kipekee ambacho kina tutofautisha na wengine ambacho hata viumbe wengine hawana. Licha ya binadamu huyu kupendelewa lakini bado wengine wanaendelea kuishi maisha ya tabu sana …

Usifanye Kosa Hili Katika Fedha Zako

Hakuna utumwa mbaya kama wakufurahisha watu ambao hata hawajali. Watu wengi wamekuwa wakikaza kufurahisha watu ambao hata hawajali. Tumekuwa na maisha ya utumwa ya kutaka kuonekana kwa nje sisi ni watu bora kwa kununua vitu vya gharama ili tuonekane na sisi ni watu tunaokwenda na fasheni. Wengine hata wanadiriki kwenda kukopa ili tu maisha yake …

Ukitaka Kujua Tabia Ya Mtu Mchunguze Kwenye Maeneo Haya Mawili

Haiba ni tabia ya mtu yaani jinsi ulivyo hivyo tabia yako ndiyo haiba yako ilivyo. Ukitaka kujua asili ya mtu ni mtu wa namna gani basi endelea kusoma hapa. Huwezi kujua tabia ya mtu kama hujakaa naye vizuri, unaweza ukawaona watu ni wastarabu sana kwa nje lakini kwa ndani ni watu wakorofi sana. Mara nyingi …

Jinsi Wafanyabiashara Wanavyofukuza Wateja Wao

Hawajakosea wahenga waliposema mteja ni mfalme. Hivi unajua mfalme ni mtu anayetaka kile anachokitaka yeye bila sababu yoyote kwa sababu ni mfalme. Mfalme hajiulizi nitapate kitu fulani ila yeye akitaka kile anachokitaka anakipata ndivyo hivyo ulivyo. Maisha yetu kwa kiasi kikubwa yametawaliwa na biashara, huwezi kupita sehemu na ukakosa kuona watu wakifanya biashara. Biashara zilikuwepo …

Hivi Ndivyo Unavyojijengea Hali Ya Kuvumilia Au Kufurahia Maisha Yako

Wanafalsafa wamekuwa wakituambia kuwa uko hivyo ulivyo kulingana na kile unachofikiri. Wengine hawaamini lakini ndiyo ukweli uhuo, akili zetu ni kama sumaku zinavuta kile ambacho kinaendana nacho. Vyote tulovyonazo leo vimetokana na nguvu ya uvutano ambayo tunayo leo na dunia huwa haimtengi mtu ila nguvu ya uvutano ndiyo inawatenga watu. Nguvu ya uvutano inatupa wale …

Changamoto Zote Za Matumizi Ya Kifedha Zinaanzia Hapa

Tunapambana kupata fedha kwa jasho lakini tunakuja kuipoteza kiurahisi. Kama hujui misingi ya fedha unataendelea kuteseka kila siku ni kama vile unachemsha mawe huku ukisubiria yaive. Huenda unapata hela lakini hujui fedha zako zinaenda wapi unabakia kumsingizia chuma ulete. Changamoto ya matumizi ya kifedha ni kubwa sana na wengi matumizi yanakuwa ni makubwa kuliko vipato …

Huwezi Kupendwa Na Watu Kama Hujafanya Kitu Hiki…

Muda mwingine sisi binadamu tunakuwa na unafiki kwa mfano, mtu anapokuwa hai wala hatumpi sifa zake tunasubiri pale anapokuwa mfu ndiyo tunaanza kumpa sifa nyingi kupita maelezo. Laiti kama sifa ambazo tunazowapa marehemu wetu tungekuwa tunawapa wakiwa hai huenda hata wangekuwa wanakufa huku wakifurahia na kutabasamu kwamba maisha yao yalikuwa yana maana hapa duniani kupitia …

Maisha Ya Kila Mtu Yanatakiwa Yawe Hivi…

Ukijaribu kuangalia maisha ya watu wengi lazima utakuta kuna maeneo ambayo yamepewa kipaumbele kuliko maeneo mengine. Siku zote ukiegemea kwenye kitu kimoja sana lazima mambo mengine yataenda mrama tu. Tumekuwa na maeneo mengi katika maisha yetu lakini maeneo haya katika maisha yapo katika utatu huu ambao ni maisha ya kiroho, kimwili na kiakili. Haya maisha …

Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Ili Mtoto Wako Awe Bora.

Hakuna mtu aliyewahi kuandika barua kuzaliwa  ya kuomba kuzaliwa. Hakuna mtu aliyeomba kuzaliwa na mzazi ambaye anaye sasa lakini sisi sote tumejikuta tumezaliwa na wazazi ambao tunao sasa. Kumbe basi mzazi ni zawadi kutoka kwa Mungu. Wazazi wengi wa siku wanapambana kweli kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule nzuri wengine wanasema kabisa hawezi akapata taabu kama …

Mbinu Mbili Za Kutumia Pale Unapokutana Na Hali Ngumu Ya Kifedha

Hakuna kitu kinachowasumbua watu wengi kama changamoto za kifedha. Fedha imekuwa ni jawabu la mambo yote kwa kila mtu hivyo mtu akikosa fedha na maisha yake hayawezi kwenda kama vile anavyotaka yeye. Kila mtu ana shida ya hela ndiyo maana kila siku tunapambana ila shida iko kwa yule mtu ambaye hapambani maana ni ngumu kupata …

Design a site like this with WordPress.com
Get started