Njia Pekee Ya Kuwafanya Watu Wakupe Kile Unachotaka

Mafanikio yoyote yale tunayotaka kwenye maisha yetu tayari yako kwa wengine. Chochote tunachofanya tunawategemea wengine ili nasi tuweze kufanikiwa. Kumbe basi, kama tunataka kufanikiwa kwenye kile unachofanya anza kuwasaidia wengine kupata kile wanachotaka. Mwanasaikolijia Sigmund Freud aliwahi kunukukiwa akisema kile ambacho watu wanakifanya kinasukumwa na tamaa mbili, ngono na ukuu. Mwanafalsafa John Dewey anasema hitaji …

Usiache Kufanya Kama Unaweza

Usikubali kuishi maisha ambayo hayana maana ndani kwako, maisha mazuri ni yale ya kuishi kusudi la maisha yako. Changamoto kubwa iko katika kujua kusudi la maisha yako, na hili ndilo linawafanya watu wengi mpaka wanakufa bila kujua haswa nini wanataka kwenye maisha yao. Kwenye kitabu cha Ongea Lugha Yako, sikiliza sauti yako ya ndani ndiyo …

Usiogope Kuuliza Kitu Hiki Kwenye Maisha Yako

Kuuliza siyo ujinga. Unapokuwa una safari kwenda sehemu usiyojua yaani wewe unakuwa mgeni huwezi kuona aibu wala kuogopa kuuliza.Lazima utauliza ili usije ukapotea lakini pia uweze kufika kule unakotaka kufika. Unapokuwa hujui kitu, usiogope kuuliza kitu. Hakuna mtu anayejua kila kitu, hivyo unapomuuliza mtu atakujibu kama kipo ndani ya uwezo wake.Na mara nyingi watu wanapenda …

Usimchinje Ng’ombe Wako Kwa Oda Ya Maini

Ni watu wa chache sana wanaishi maisha wanayotaka kwa sababu wengi hawaishi vile wanavyotaka bali wanaishi vile wanavyotaka wengine. Je hayo maisha unayoishi ndiyo maisha yako halisi? Huwa tunaigiza maisha yetu mchana lakini ikifika usiku huwa tunakutana na sisi wenyewe tunajiona kabisa ni watupu na kile tunachofanya siyo sahihi. Utaweza kuwadanganya watu wote lakini huwezi …

Tatizo Lako Liko Hapa

Kama unapata maarifa ya kukuwezesha kuwa bora basi unatakiwa kuwa bora kweli. Usipokuwa bora utakua huna tofauti kabisa na yule mtu ambaye hajifunzi. Kwa chochote kile unachojifunza jaribu kubadilika hata watu unaoishi nao waone kweli una kitu cha tofauti ndani yako. Tatizo lako ni kwamba uko hivyo ulivyo kwa sababu ya kutochukua hatua sahihi. Kwa …

Hii ndiyo Njia rahisi kuliko zote duniani za kuwa tajiri

Wote tunajua kuwa ni jinsi gani fedha ilivyokuwa muhimu kwenye maisha yetu. Inatusaidia kuendesha maisha yetu na kulipa bili mbalimbali. Fedha ni muhimu kweli na hilo halina ubishi hata kidogo. Kila mtu anatamani awe na uhuru wa kifedha wa kumwezesha kufanya kile anachotaka na watu wengi hawana uhuru wa kifedha na dalili moja wapo ya …

Huyu Ndiye Mtu Mchafu zaidi Duniani

Ukistaajabu ya Musa utayaona ya …, Duniani kuna mambo na kila kitu kipo kwa ajili ya kukamilisha dunia. Hakuna uchafu bila usafi haya yote yako kwa ajili ya kukamilisha dunia. Nilistaajabu jana kujua kuna mtu mchafu zaidi duniani nikaona leo nikushirikishe jambo hili huenda kukawa na kitu cha kujifunza. Amou Haji ni raia wa Irani …

Hiki Ndicho Unachotakiwa Kujali

Kuna mtu akiangalia historia yake ya maisha ilivyo anaweza kusema kuwa yeye hawezi kufanya kitu kadiri ya historia yake. Tunayo mifano ya watu wengi tu tokea enzi na enzi ambao walikuwa na historia mbaya lakini Mungu alikuja kuwabadilisha na kuwa watu wa historia nzuri. Ndiyo maana leo ninakuambia rafiki yangu, haijalishi unatokea wapi?, Kinachojali ni …

Mambo Mawili Unayopaswa Kuwa Nayo Ili Kutenda Miujiza Kwenye Maisha Yako

Kila mmoja wetu amezaliwa na uwezo mkubwa sana ndani yake lakini kadiri ya mazingira tunayoishi, mitazamo hasi tunayoingiza akilini inasababisha kushindwa kutumia uwezo mkubwa wa akili tulio nao. Wewe ni kiumbe uliyependelewa kuliko viumbe vilivyoko duniani lakini cha ajabu yake hutumii vema upendeleo huo ambao umejaliwa kuwa nao. Hivi ukijiuliza tunakwama wapi mpaka tunashindwa kufanya …

Unachokihofia Huwa Hakipo

Huwa tunatengeneza mazingira ya hofu ambayo hata haipo katika hali ya kawaida. Unakuta mtu anatengeneza mazingira ya hofu kiasi kwamba inamletea hata kushuka kwa ufanisi wake wa kazi. Pengine unajua siku fulani utakuwa na tukio fulani basi mtu anatengeneza mazingira ya hofu, anaanza kuiwazia hiyo siku itakuwaje na matokeo yake anaanza kujawa na hofu ambayo …

Design a site like this with WordPress.com
Get started