Epuka Kitu Hiki Kama Unahitaji Kufanikiwa

Mafanikio yoyote yale unayojua hayapatikani kirahisi. Kila mafanikio unayopata ujue umeweka kazi. Kama ingekuwa mambo ni marahisi, kila mtu angefanya. Ukitaka kufanikiwa kwenye kile unachotaka epuka demokrasia. Demokrasia haiwezi kukupa kile unachotaka kwenye maisha yako. Usijipe sababu za kidemokrasia kama unataka kufanikiwa. Demokrasia inabembeleza. Na mafanikio hayahitaji kubembeleza bali yaani hitaji lazima. Kama unataka kupiga …

Sehemu Nzuri Ya Kuanzia Kuuza

Usifungue biashara kisha ndiyo uanze kutatuta wateja. Hapa ndiyo mahali ambapo watu wengi wanakosea. Kabla hujafungua biashara hakikisha soko linakujua. Na unapofungua biashara inakua ni ukamilifu wa biashara yako. Soko limeshakujua kwahiyo kazi ni kufanya kazi. Ni kazi kufanya biashara kama soko halikujui. Na soko huwa halina huruma. Kama hujajitangaza na kukujua vizuri utalilaumu bure …

Mbinu Itakayokusaidia Kupunguza Matatizo Ya Ndoa Yako

Hakuna nyumba ambayo utaenda utakuta wamebandika bango lao kubwa mlangoni likisema kuwa HAPA HAKUNA MATATIZO YA NDOA.Hakuna familia ambayo haipitii majaribu kama bado iko hai. Sehemu pekee ambayo haina changamoto ni kaburini, ukifa utakua umejitenganisha na shida za duniani. Watu wanazidi kuwa na mitazamo hasi sana juu ya ndoa. Familia za mama mmoja yaani single …

Kiapo Cha Kuianza Siku Yako Na Siku Ya Mwisho Ya Kupata Kitabu Cha Kwa Nini Umezaliwa Kushinda Kwa Bei Ya Ofa

Mpendwa rafiki yangu, Ukurasa wa sita wa kitabu hiki ambacho utakwenda kukisoma utakutana na kiapo cha siku yako yaani positive declaration Hiki ni kiapo ambacho kitakusaidia kuinza siku yako kwa ushindi mkubwa. Maana kuna nguvu kubwa sana ya kuapa wewe hushangai kwanini watu huwa wanaapa wakati wa kuweka nadhiri, ndoa, kazi n.k? Unapoapa unakuwa unajiunganisha …

Haya Ndiyo Mapambano Ambayo Hutakiwi Kupigania

Rafiki, Siyo kila mapambano yana faida kwako. Siyo kila mapambano yanakuja kwako unatakiwa kuyapigania. Kabla hujaingia kwenye pambano lolote lile, jiulize je haya mapambano yana faida kwangu? Kwa mfano, unaingia kwenye pambano na kupigana eti kwa sababu kuna mtu hajakusalimia, au umemsalimia hajaitikia. Unaanza kujiambia kuwa fulani anajisikia ndiyo maana hajaitikia salamu yangu au ndiyo …

Je Unajua Ushindi Huwa Unaanza Na Kuanza? (Utaratibu Wa Kupata Kitabu Cha Kwa Nini Umezaliwa Kushinda)

Huwezi kupata ushindi wowote katika maisha yako kama hujaanza kufanya kile unachotaka. Unapochukua hatua ya kwanza kwenye kitu chochote kile ni kama kuondoa laana. Kumekuwa na laana ya watu wengi kwenye eneo la kuanza. Ukitaka kupata kile unachotaka, anza kwanza kukifanyia kazi. Unapoanza usiangalie matokeo gani utapata, wewe chukua hatua ambacho ndiyo kitu kilichopo ndani …

Huu Ndiyo Wasifu Mzuri Unaopaswa Kuuacha Duniani (CV)

Kitu pekee ambacho unatakiwa kufanya hapa duniani kabla hujafa ni kurefusha CV au wasifu wako. Kuna wasifu mwingine ni wa kibinafsi sana hauwezi kusomwa mbele ya watu. Wasifu wa kibinafsi huwa unagusa maisha yako tu na familia yako. Hebu jiulize miaka 50 ijayo utaitwa mzee nani? Dunia itajivunia nini kutoka kwako? Nyumba nzuri uliyojenga, au …

Ukitaka Kuwaelewa Wengine Fanya Hivi

Jaribu kuvaa viatu vyao na kutembea kwenye viatu hivyo. Unaweza ukawa unamlaumu mtu au unamhukumu mtu lakini ukivaa viatu vyake na kutembea kwenye viatu hivyo ndiyo utajua kile anachosema ni nini. Kifupi, jiweke kwenye nafasi ya wengine na fikiri na kufanya kwa namna wanavyofanya wao utawaelewa vizuri kwa nini wanafanya kile wanachofanya. Kuna wengine kile …

Kabla Hujaanza Mambo Makubwa Hakikisha Unafanya Mambo Haya Muhimu

Mtu akifunga kula iwe ni kwaresma, mwezi wa ramadhani au siku yoyote ile ambayo amejipangia kufunga kwa sababu zake za kiroho pale anapofungua mfungo wake huwa haanzi kwa kula ugali mgumu. Ila ataanza kunywa vitu vya moto kama vile uji au chai kwa ajili ya kufungua tumbo. Kwanini sasa mtu amekaa na njaa muda wote …

Usiingie Kwenye Mtego Huu

“Chukua tu halafu utanilipa mwisho wa mwezi”Ni mtego mbaya ambao watu wengi huwa wanaingia. Usitumie fedha ambayo hujaipata kununulia vitu. Maana unatengeneza shida kubwa. Usikubali mtu akuambie chukua halafu utalipa mwisho wa mwezi. Unatengeneza deni kubwa ambalo linakuja kukutesa hapo baadaye katika ulipaji. Kutumia fedha ambayo hujaipata kwa lugha rahisi ni kukopa. Ushauri mzuri wa …

Design a site like this with WordPress.com
Get started