Kuwa Wa Kwanza Na Wa Mwisho Katika Sehemu Hizi Mbili

Mpendwa rafiki, Ili kujitofautisha na wengine unatakiwa uwe na nidhamu sana kwa sababu mtu mwenye nidhamu ya maisha anakuwa siyo mtu wa kuongea bali ni vitendo hivyo basi, yule anayesimamia nidhamu anakuwa anatekeleza mambo mengi katika maisha yake. Huwa tunapenda kuwa kama watu fulani kwa mdomo tu lakini sasa kuingia katika uwanja wa kufanya ndiyo …

Ondoka Haraka Sana Kama Uko Katika Hali Hii Ya Kifedha

Mpendwa rafiki yangu, Kuna ndugu mmoja alifiwa na rafiki ya mama yake hivyo huyo ndugu alishindwa kwenda kumzika rafiki wa mama yake kwa sababu ya kukosa pesa kabisa. Labda ingekuwa nauli ya mkoa kwa mkoa lakini ni ndani ya mkoa hapo tunamaanisha ni kama tu kupanda daladala ndani ya mkoa unaoishi yaani kutoka wilaya moja …

Utafanikiwa Kwa Njia Zote Lakini Siyo Hii

Mpendwa rafiki, Mafanikio ni mazuri lakini sharti upitie njia sahihi. Kama unataka kuwa na mafanikio makubwa ya kibiashara au uwekezaji wowote ule hauwezi kukwepa kitu kinachoitwa kodi. Huwezi kuishi kwa kukimbia kila siku kwa kukwepa kulipa kodi pamoja na kurasimisha biashara zako. Mara nyingi halali yoyote ni kama ukweli unatuweka huru na kufanya mambo yetu …

Kitu Pekee Unachojidhulumu Katika Zama Hizi

Mpendwa rafiki, Ukiingia katika jamii yetu na ukikaa na watu waliokata tamaa utaona duniani si sehemu salama ya kuishi kwa kila mmoja wetu. Utaambukiwa virusi vya watu waliokata tamaa na kuona maisha ni magumu sana na watu ambao wanalalamika kuwa maisha ni magumu ni wale ambao hawachukui hatua ipasavyo yaani hawajitumi. Kwa sababu maisha ni …

Njia Bora Ya Kuona Mchakato Wowote Ni Mrahisi

Mpendwa rafiki, Kila mtu anapitia mchakato fulani katika maisha yake. Kila mtu anapambana kila siku kupata kile anachokitaka kwenye maisha yake. Maisha yanakosa hamasa kama unakuwa huna kitu unchokitafuta lakini ukiwa na kitu kinachokupa hamasa ni kusukuma kwanini ufanye kila siku, kwanini usiahirishe, usiweke sababu bali matokeo tu. Unatakiwa uwe na kitu ambacho kinakusukuma kila …

Mambo Matatu Ya Kujifunza Kutoka Ndege Aina Ya Tai

Mpendwa rafiki yangu, Kama uko duniani basi kujifunza ni wajibu wa kila mtu. Ukikwepa kujifunza basi unakwepa maisha yako, huwezi ukafanikiwa kama unakwepa kujifunza kwenye maisha yako. Ni wazi kwamba kila mmoja wetu amezaliwa akiwa anajua vitu viwili tu kulia na kunyonya maziwa ya mama. Lakini leo hii tunajua vitu vingi zaidi ya hivyo na …

Jinsi Ya Kuepuka Kutosahau Vitu Ndani Ya Siku Yako

Mpendwa rafiki, Hongera sana kwa juma jipya na siku bora sana ya leo katika maisha yako. Binadamu huwa tunakuwa na asili ya kusahau mambo sana, huwa tunajikuta tunaahidi kufanya mambo mengi na wakati mwingine tunawaahidi hata watu kuwa nitafanya kitu fulani lakini baada ya muda tunajikuta tunasahau. Muda mwingine tunabanwa kweli hata tukiona jumbe katika …

Kitu Ambacho Hutakiwi Kujiharibia Kwenye Maisha Yako

Mpendwa rafiki, Maisha ni magumu tayari ila watu wanayafanya kuwa magumu zaidi. Hakuna kitu karahisi katika hii dunia yaani kila kitu unaalikwa kulipia gharama ili uweze kukipata. Watu wanasema maisha ni magumu je kuna siku ulishawahi kusikia maisha ni marahisi? Maisha ni magumu kwa kila mmoja kwa sababu ili upate lazima upambane katika ile dhana …

Kitu Muhimu Cha Kuzingatia Kabla Hujachukua Mkopo

Mpendwa rafiki, Kuna mikopo ya aina mbili yaani mikopo inayozalisha na mikopo isiyozalisha. Kwa mfano, unakopa kwa ajili ya kununua nguo na mikopo ya kuzalisha ni pale unapokopa kwa ajili ya kwenda kuboresha kile unachofanya yaani biashara yako. Lakini watu wengi wanachukua mikopo ambayo haizalishi ndiyo maana mikopo inaendelea kuwa sumu kwa watu wengi kwa …

Mtego Mbaya Unaotuingiza Katika Mazoea Ya Kila Siku

Mpendwa rafki, Hakuna eneo la maisha yetu ambalo linaweza kwenda vizuri bila kuwa na nidhamu binafsi. Tumekuwa ni watu wazuri wa kupika sababu nzuri za kwanini hatuwezi badala ya kwanini tunaweza. Tunapanga kufanya mambo mengi tena ni mazuri na makubwa lakini tunashindwa kutekeleza kile tunachopanga kwa sababu ya kukosa nidhamu binafsi. Tukikosa nidhamu tumekosa maisha …

Design a site like this with WordPress.com
Get started