Ni familia yako. Pata picha ukiumwa au ukipata tatizo ni nani anakua yuko tayari pamoja na wewe? Ni familia yako. Ukiumwa familia yako ndiyo inayopambana kuhakikisha unakua bora lakini watu wa nje hawatakua na habari na wewe. Kwa mfano, mke au mume ukiumwa atakayekuhangaikia ni mke au mume wako lakini siyo mchepuko wako. Hapo unapata …
Category Archives: MAHUSIANO NA NDOA
Jinsi Ya Kumpandisha Bei Mwenza Wako
Kadiri ya uzoefu wangu wa kujifunza na huduma ninayotoa kwenye eneo la mahusiano na yale ninayokutana nayo kwenye jamii nimekuja kuona kwamba baadhi ya Wanandoa wanashushana bei. Inakuwaje mpaka mtu anamshusha bei mwenza wake? Ni pale mwenza anapokuwa hampi mwenza wake thamani anayostahili kupata. Kwa mfano, kumsema mwenza wako kwenye kadamnasi huko ni kumshusha bei. …
Jinsi Ya Kulainisha Mahusiano Yako
Mahusiano yetu yanakuwa magumu wakati mwingine kwa sababu kuu moja ambayo ni kukosa mawasiliano. Kama unavyojua kitu kikiwa kigumu kinatakiwa kilainishwe ili kupatikana kwa ulaini. Mahusiano yetu yanakuwa magumu endapo yakikosa mawasiliano mazuri. Kitu ambacho kinaweza kulainisha mahusiano yetu ni mawasiliano na wale ambao tunahusiana nao. Kila unayehusiana naye anahitaji muda wako na usipompatia muda …
Hii Ndiyo Njia Nzuri Ya Kuwapenda Watu
Njia bora kabisa ya kuwapenda watu ni kuwakubali kama walivyo. Kila mtu ana tabia zake, kila mtu ana upekee wake, uimara na udhaifu wake. Tunaweza kunufaika na wale watu wetu wa karibu kwa kuwapenda kama walivyo. Aliyekuwa raisi wa Marekani Abraham Lincoln aliwahi kunukuliwa akisema, ukitafuta ubaya kwa mtu tegemea kuupata. Kazi yetu siyo kutafuta …
Ili Uweze Kufanikiwa Kwenye Safari Ya Mafanikio Makubwa Lazima Mwenza Wako Akupe Kitu Hiki
Watu ambao wako kwenye ndoa huwa wanakutana na upinzani mkubwa hususani pale mmoja wa ndoa anatapotaka kuthubutu kitu au anapokuwa na ndoto kubwa. Kikawaida jamii zetu hawapendi kuona mtu akiteseka kwa mfano, ukimwambia mtu kwamba unataka kwenda kufungua biashara na yeye hafanyi biashara atakuambia biashara ni hatari, usijitese. Na watakuambia hivyo ili mradi tu wasikuone …
Waepuke Marafiki Hawa Wawili Na Kuwa Na Rafiki Huyu Tu
Urafiki ni kitu muhimu sana kwenye maisha yetu. Na zana ya kujenga na kuimarisha mahusiano ni mawasiliano. Mwanafalsafa Aristotle enzi za uhai wake alisisitiza sana umuhimu wa urafiki kupitia maandiko ya kifalsafa. Na alifanikiwa kugawa urafiki kwenye ngazi tatu. Ngazi ya kwanza ni urafiki wa faida au urafiki wa nipe nikupe.Huu ni urafiki ambao unajengeka …
Continue reading “Waepuke Marafiki Hawa Wawili Na Kuwa Na Rafiki Huyu Tu”
Siwezi Kuishi Bila Yeye, Kwa Sababu Yeye Ndiyo Kila Kitu Kwangu
Ni kauli za watu ambao wako katika mahusiano ya kimapenzi. Lakini siyo kweli, eti kwamba huwezi kuishi bila yeye kwa sababu yeye ndiyo kila kitu kwako. Alikuambia nani dunia iko hivyo? Usipende kujipa vizuizi vingi kwenye maisha yako, maisha tayari ni magumu na wewe unayafanya kuwa magumu zaidi kwa kujiongezea mzigo kwamba huwezi kuishi bila …
Continue reading “Siwezi Kuishi Bila Yeye, Kwa Sababu Yeye Ndiyo Kila Kitu Kwangu”
Jinsi Ya Kuendelea Kumpenda Mwenza Wako Wa Ndoa
Wako ambao wamefikia hatua ya kuwachukia na kuwachoka wenza wao wa ndoa ili hali mwanzo walikuwa wanapendana kama kawaida. Kama mtu ataamua kumchukia mwenza wake wa ndoa maana yake atakua amevua upendo wa kweli na kuanza kujichukia yeye mwenyewe. Watu wanachokana mapema kwa sababu waliingia kwenye ndoa wakiwa na matarajio binafsi ambayo wangeyakuta kutoka kwa …
Continue reading “Jinsi Ya Kuendelea Kumpenda Mwenza Wako Wa Ndoa”
Epuka Kujikaanga Na Mafuta Yako Mwenyewe
Unajikaanga na mafuta yako mwenyewe pale unapokuwa unamchukia mtu bila sababu yoyote ile. Muda mwingine hata yule unayemchukia hajui hilo yeye anaendelea na maisha yake huku wewe ukiendelea kuteseka. Chuki ni sawa na kunywa sumu ili kumkomoa mtu mwingine kitu ambacho unaishia kujiumiza wewe mwenyewe. Hisia ya chuki ni mbaya sana kwa sababu haina faida …
Endelea Kufanya Mambo Haya Yanayodumu Milele
Endelea kufanya mambo mazuri yanayodumu milele. Katika zama tunazoishi unaweza ukafanya mambo mazuri na ukaona hakuna anayejali. Lakini huo siyo ukweli, mambo mazuri unayofanya hata kama ni kidogo kiasi gani huwa yanagusa maisha ya wengine na huwa wengine hawayasahau. Kwa mfano, mwandishi Robin Sharma katika kitabu chake cha Manifesto, the hero every day anatushirikisha hadithi …
Continue reading “Endelea Kufanya Mambo Haya Yanayodumu Milele”