Wauzie watu kile ambacho watu tayari wanataka.
Usijisumbue kuwauzia watu kitu ambacho hawakitaki. Huko ni kupingana na asili.
Ni kupingana na soko, mara zote soko huwa halina huruma hivyo linampiga yeyote anayekwenda kinyume na soko.
Kwa mfano, ulaji wa vitoweo, huhitaji nguvu KUBWA kumshawishi mtu kula kuku.
Lakini, Unahitaji nguvu KUBWA kumshawishi mtu kula kware.
Hapo unajifunza nini? Wauzie watu kile ambacho wanataka na siyo kile ambacho wewe unataka.
Kabla hujafanya kile unachotaka kufanya, jiulize watu wana uhitaji wa kile unachouza?
Usipingane na asili, utaumia bure.
Kama hujalalamika biashara ngumu, jiulize je, kile unachouza watu wanakihitaji tayari au unatumia nguvu kuwashawishi wateja kununua? Chukulia mfano wa kuku na kware.
Hatua ya kuchukua leo; angalia watu wanataka nini kisha kuwa tayari kuwapa kile wanachotaka.
Kumbuka, kwenye kila fursa, jiulize watu wana uhitaji wa kile unachouza?
MUHIMU;
Kama bado hujajiunga na kundi la wasapu la Mimi ni Mshindi jiunge leo kwani kuna maarifa mengi unayakosa ambayo sikushirikishi hapa.
Kujua ni maarifa gani hayo na jinsi ya kujiunga nitumie ujumbe wasapu kwa namba 0717101505. Kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha ya kiswahili wasiliana kwamba namba 0717101505.
Rafiki Na Mwalimu Wako, Afisa Mhamasishaji Mkuu (CIO)Chief Inspiration Officer.
Mwl. Deogratius Kessy
0717101505 au 0767101504
https://kessydeo.home.blog