Design a site like this with WordPress.com
Get started

Sala Dhidi Ya Kuwasema Wengine Vibaya

Usiwaongelee  wengine  vibaya, najua kuna watu wengine hawawezi kumaliza siku bila kuwasema WENGINE vibaya.

Midomo yao iko kama vile bata ambaye hawezi kujizuia pale anapotaka kujisaidia.

Nakusihi sana acha kusema watu vibaya, wewe siyo kiranja wa dunia ambaye unataka watu wawe kama vile unavyotaka wewe.

Ukikosa mazuri kwa mtu ya kusema, basi kaa kimya na siyo lazima kuongea.

Benjamin  Franklin amewahi  kunukuliwa  akisema sitamwongelea  mtu  mwingine  vibaya : “Kamwe nitasema  yote  mazuri ninayoyajua  kuhusu  wengine.”

Kauli  hiyo  imebeba  msingi  muhimu sana  kwenye  kuaminika  ambao  ni  kutokuwaongelea  wengine  vibaya.

Ukitaka kuaminika na wengine, kamwe usiwaongelee wengine vibaya bali sema yale ambayo ni mazuri tu kutoka kwao.

Hatua ya kuchukua leo;
Sali sala hii kila siku;
sitamwongelea  mtu  mwingine  vibaya , kamwe nitasema  yote  mazuri ninayoyajua  kuhusu  wengine.

Kwahiyo, sema mazuri unayoyajua kuhusu wengine.

MUHIMU;
Kama bado hujajiunga na kundi la wasapu la Mimi ni Mshindi jiunge leo kwani kuna maarifa mengi unayakosa ambayo sikushirikishi hapa.

Kujua ni maarifa gani hayo na jinsi ya kujiunga nitumie ujumbe wasapu kwa namba 0717101505. Kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha  ya kiswahili wasiliana kwamba namba 0717101505.

Rafiki Na Mwalimu Wako, Afisa Mhamasishaji Mkuu (CIO)Chief Inspiration Officer.

Mwl. Deogratius Kessy

0717101505 au 0767101504
https://kessydeo.home.blog

Leave a comment

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

%d bloggers like this: