Design a site like this with WordPress.com
Get started

Hiki Ndiyo Kitu Ambacho Hakijawahi Kumuangusha Mtu

Rafiki,

Ni kawaida katika jamii yetu watu kuona kama vile kazi ni mateso sana.
Watu kufanya au kutimjza wajibu wao wanahisi kama vile ni utumwa na siyo sehemu ya maisha yao.

Tukianzia katika kuamka mapema , mtu akiwa bize na kazi zake wako watakaosema fulani anateswa au anajitesa na kazi.
Hapa tunajifunza kuwa licha ya kuwa kazi ni muhimu sana tena ni rafiki yetu kwa sababu kazi inatusaidia kupata kile tunachotaka katika maisha yetu.

Lakini kuna watu hawapendi kazi, wanahisi kazi ni kama utumwa.
Kazi siyo utumwa bali kazi ni asili ya binadamu tangu kale.

Kitu ambacho hakijawahi kumuangusha mtu katika kazi ni juhudi.
Watu wenye bidii kwenye jambo lolote lile hufanikiwa sana katika kile wanachofanya.

Kama unataka kufanikiwa weka bidii na juhudi utapata matokeo mazuri.
Watu wanajituma sana katika kazi zao na huwa juhudi inamlipa mtu kadiri anavyojitoa.

Jitume utafanikiwa, jali kazi, jali kile ambacho kinakuingizia fedha haya mengine achana nayo.

Uwe rafiki wa kazi, acha kuwa mtumwa wa mambo yasiyochangia faida chanya kwenye maisha yako.

Kama ukiweka juhudi katika kazi, juhudi itakuzawadia matokeo mazuri na wala haijawahi kumuangusha mtu.

Hatua ya kuchukua leo; Juhudi katika jambo lolote ndiyo msingi wa mafanikio.

Kwahiyo, kama unataka kufanikiwa katika jambo lolote lile , nakusihi weka juhudi na utakua na mafanikio mazuri sana kwenye kile unachofanya.

Kila la heri rafiki yangu.

Rafiki na mwalimu wako,
Mwalimu Deogratius Kessy
http://www.mtaalamu.net/kessydeo

Published by Deogratius Kessy

Mwandishi,mwalimu na mjasiriamali. Unaweza kutembelea Blog yake ya www.kessydeo.home.blog kujifunza zaidi na unaweza kuwasiliana naye kwa namba 0717101505/0767101504 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com

Leave a comment

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

%d bloggers like this: