Design a site like this with WordPress.com
Get started

Mbinu Bora Ya Kuishi Maisha Yako Na Kuwa Na Mafanikio Makubwa

Mpendwa rafiki yangu,

Huenda kuna watu tokea wazaliwe hawajawahi kuishi maisha yao. Kuishi maisha yako ni kuishi vile upendavyo wewe na sasa hiyo imekuwa ni changamoto ya watu wengi. Kuna gharama za kuishi maisha yako, hivyo kama unataka kuishi maisha ukubali kuzilipa mapema.

Maisha bora ya kuishi maisha yako iwe ni kwenye kazi, biashara na nk ni haya;

Sema kile unachotaka kusema,

Sema kile unachotaka kusema ambacho unajua ni sahihi kwako,fanya tena kile ambacho unataka kufanya ambacho unaamini ni sahihi kwako.

Huwezi kumfurahisha kila mtu ila unaweza kujifurahisha wewe mwenyewe tu hapa duniani na unaweza kujifurahisha vile utakavyo.

Watu wengi wanashindwa kusimama imara katika maisha yao. Hawajiamini katika kile wanachotaka kufanya na kil wanachokijua na hiki ndiyo hupelekea watu wengi kushindwa kuishi maisha yao.

Unapotaka kuishi maisha yako ishi vile utakavavyo na siyo watakavyo watu. Unatakiwa kusimama kwa miguu yako mwenyewe. ukiwategemea watu lazima watakuangusha katika kutekeleza kile unachotaka kuishi.

SOMA; Vishinde Vitu Hivi Vitatu Na Maisha Yako Yatakuwa Bora Sana

Kuwa na maoni yako hata kama wengine watakupa maoni yao. Kila mmoja wetu anatakiwa kuishi kadiri ya maoni yake mwenyewe na siyo maoni ya watu. Tujifunze kuamua na kuishi maoni yetu na siyo ya watu wengine. Jiamini kwenye unachotaka kusema, kuandika ili mradi tu ni sahihi.

Huwezi kuwa mtu bora na mwenyewe mafanikio kama huyaishi maisha yako kikamilifu na umewapa watu wengine nafasi ya kuamua kile wanachotaka wao na siyo kile unachotaka wewe.

Usiogope rafiki yangu, maisha ni mafupi ukiwa unamhofia kila mtu atasemaje juu yaw ewe, unachotakiwa kufanya ni kuishi vile uwezavyo na usiwasikilize wanasema nini.

Hatua ya kuchukua leo; ishi vile upendavyo wewe na siyo wapendavyo watu. Sema kile unachotaka kusema ambacho unajua ni sahihi kwako. Fanya kile unachotaka kufanya ambacho unakiamini na unaona ni sahihi.

Kwahiyo, kama unaishi maisha yako bila kuvunja sheria huna shida na mtu yeyote. Kuishi maisha yako zingatia kutokwenda kinyume na sheria za mahalia.

Muhimu; kama bado hujajiunga na kundi la wasapu la mimi ni mshindi jiunge leo kwani kuna maarifa mengi unayakosa ambayo sikushirikishi hapa. Kujua ni maarifa gani hayo na jinsi ya kujiunga bofya hapa au nitumie ujumbe wasapu kwa namba 0717101505. Kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha ya kiswahili bonyeza hapa.

Ukawe na siku bora sana rafiki.

Rafiki na mwalimu wako,

Deogratius kessy

0717101505/0767101504

deokessy.dk@gmail.com // kessydeo@mtaalamu.net

Asante sana

 

Published by Deogratius Kessy

Mwandishi,mwalimu na mjasiriamali. Unaweza kutembelea Blog yake ya www.kessydeo.home.blog kujifunza zaidi na unaweza kuwasiliana naye kwa namba 0717101505/0767101504 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com

Leave a comment

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

%d bloggers like this: