Design a site like this with WordPress.com
Get started

Huu Ndiyo Muda Ambao Hauna Foleni Kabisa Kwenye Maisha Yako

Mpendwa rafiki yangu,

Kwa wale wanaoishi katika majiji kitu kinachoitwa foleni imekuwa ni kitu cha kawaida sana. lakini mimi siko hapa kukushirikisha foleni ya barabarani. Muda wetu umekuwa mfupi sana na mambo ya kufanya ni mengi sana tunajikuta tunajiambia tutafanya kesho na kesho imekuwa kesho mpaka mwaka unaisha.

Mambo siyo marahisi kama unavyofikiria ila inawezekana kama ukiamua. Kama mambo yamekuwa mengi una muda mchache inabidi sasa upunguze mambo ambayo hayana umuhimu kwako na uelekeze nguvu kubwa katika yale mambo muhimu tu. Huna muda wa kufanya kila kitu ila una muda wa kufanya mambo muhimu tu.

Muda mzuri ambao hauna foleni katika maisha yako ni asubuhi na mapema.  Kama siku ikianza wewe unakosa muda yaani mambo ni mengi unakua na foleni nyingi hivyo unashindwa kufanya mambo yako basi amka asubuhi na mapema. Muda wa alfajiri ni muda ambao hauna hata foleni muda ambao wengine wamelala yaani dunia inakua imelala hivyo kuna kuwa na utulivu mkubwa sana wa kufanya mambo yako.

Amka asubuhi kuanzia saa 10 alfajiri ianze siku yako, kile kitu ambacho ni muhimu kwako anza kukifanya. Anza kujitumikia wewe mwenyewe muda huo kabla dunia haijaamka umeshamaliza kufanya mambo yako yote muhimu.

SOMA; Huu Ndiyo Muda Mzuri Wa Kujipatia Ushindi Wa Uhakika

Wale ambao wanasema hawana muda wa kusoma, kufanya mazoezi, kuandika, kufanya kitu cha ziada kwa ajili ya maisha yako basi muda upo. Acha kitanda na nenda kajitumie kwanza wewe mwenyewe, ni aibu sana kukurupuka kutoka kitandani na kwenda kuwatumikia wengine kabla yaw ewe kujitumikia.

Anza siku yako mapema, ipangilie itakuwaje, andika mipango yako yote ya siku, andika ndoto zako na nenda kaifanyie kazi. Huu muda hauna foleni unatakiwa kuutumia vizuri kwa mambo muhimu na siyo kuingia kwenye mitandao ya kijamii.

Hatua ya kuchukua leo; muda ambao hauna foleni basi ni kuanzia asubuhi ya saa kumi mpaka kumi na mbili. Unaweza kufanya mambo yako yote bila usumbufu wa dunia na mara nyingi kelele za dunia huwa zinaanza kuanzia saa moja.

Hivyo basi, kama huna muda basi punguza kulala sana na amka mapema tumia muda huo kufanya yale mambo yako binafsi yanayokusaidia katika ukuaji na maendeleo yako binafsi.

Muhimu; kama bado hujajiunga na kundi la wasapu la mimi ni mshindi jiunge leo kwani kuna maarifa mengi unayakosa ambayo sikushirikishi hapa. Kujua ni maarifa gani hayo na jinsi ya kujiunga bofya hapa au nitumie ujumbe wasapu kwa namba 0717101505. Kupata vitabu vizuri vya kujisomea kwa lugha ya kiswahili bonyeza hapa.

Ukawe na siku bora sana rafiki.

Rafiki na mwalimu wako,

Deogratius kessy

0717101505/0767101504

deokessy.dk@gmail.com // kessydeo@mtaalamu.net

Asante sana

 

Published by Deogratius Kessy

Mwandishi,mwalimu na mjasiriamali. Unaweza kutembelea Blog yake ya www.kessydeo.home.blog kujifunza zaidi na unaweza kuwasiliana naye kwa namba 0717101505/0767101504 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com

Leave a comment

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

%d bloggers like this: